Kichanga chakutwa kimetupwa jalalani huko Mlandege Iringa

Unknown     3:11 AM    

   


Ama kwa hakika ile kauli ya ubinadamu kazi wala walioileta hawakukosea maana kwasasa binadamu tumegeuka wanyama zaidi ya wanyama wenyewe,kauli hii inakuja kufutia tukio la ajabu limetoke mjini iringa na kuvuta hisia za watu waliokuwa katika eneo hilo kushuhudia kichanga hichi kisichokuwa na hatia kikiokotwa eneo la jalalani.


Mtoto huyo aliyeokotwa huko katika mtaa wa mlandege saa mbili asubuhi amekutwa tayari akiwa ameshafariki ila polisi wanamshikilia mama mmoja ambaye jina lake halikupatikana hadi tunaingia kuziandika habari hizi,polisi wamelazimika kumkamata mwanamama huyo kufuatia kauli za majirani wakimtuhumu kuwa huyo mtoto ni wake kwani alikuwa na mimba na ghafla haipo na pia uchunguzi unaonyesha kuwa ni kama anauhusika japo bado polisi hawajatowa tamko kufuatia mahojiano hayo japo waandishi wa thesuperstarstz waliopo huko iringa walifika eneo husika na baadae polisi lakini walijibiwa kuwa wasubiri hadi uchunguzi ukamilike.

Mungu ailaze roho ya kichanga huyu mahali pema peponi amin

LIKE PAGE YETU HAPA ILI UWEZE KUPATA HABARI ZETU KUPITIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK KILA SIKU.

,

Recommended

Like Us

Company

Legal Stuff

FAQ's

Blogroll

Subscribe to Newsletter

We'll never share your Email address.
© 2015 Umbeya Specially. Blogger Templates Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.