Breaking news: Muigizaji wa bongo movie ( kashi) afariki dunia leo mchana

Unknown     8:43 AM    

Muigizaji wa filamu nchini Jaji Khamis (Kashi) amefariki dunia leo  mchana  katika hospitali ya taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam.


Kashi amewahi kutamba na mchezo wa ITV, Tamu Chungu akiwa na wasanii wenzake kama Mzee Masinde,Samson na wengine.

Baada ya kupata habari hii, mwandishi wetu aliongea  na muigizaji mwenzake Monalisa ambae amethibitisha kutokea kwa msiba huo. Monalisa amesema alipata taarifa jana kwamba Kashi amelazwa hospitali akiwa amezidiwa kiasi cha kushindwa kuongea na hivyo kushindwa kujua nini kilikuwa kinamsumbua.

Naye Hemedy PHD ametweet: REST IN PEACE MUIGIZAJI MWENZETU JAJI KHAMIS KASHI….MUNGU AKULAZE PEMA PEPONI…MOVIE YA MWISHO TULICHEZA WOTE ILIKUA MATILDA!!Sad newz
LIKE PAGE YETU HAPA ILI UWEZE KUPATA HABARI ZETU KUPITIA AKAUNTI YAKO YA FACEBOOK KILA SIKU.

,

Recommended

Like Us

Company

Legal Stuff

FAQ's

Blogroll

Subscribe to Newsletter

We'll never share your Email address.
© 2015 Umbeya Specially. Blogger Templates Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.