Lulu apata bwana! Jina lake anaitwa Junior

Unknown     11:33 PM    



NYOTA wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’, ameibua jipya ambapo kwa sasa habari ya mjini ni kwamba ana bwana mpya aliyetajwa kwa jina moja la Junior, Amani limezinasa habari hizo.
Ishu hiyo ambayo ndiyo gumzo midomoni mwa watoto wa mjini ilianza kusambaa tangu Aprili 1, 2013 staa huyo alipoangusha pati ya kusherehekea siku yake ya kuzaliwa ambayo ilichukua nafasi ndani ya Ukumbi wa Hoteli ya Serena katikati ya Jiji la  Dar es Salaam.
Maneno ya mjini yanasema kuwa staa huyo amekuwa akiweka picha yake akiwa na Junior kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii huku wadau wakimpongeza kwa kumtambulisha mpenzi wake huyo.
Mbali na picha ya Lulu akiwa na huyo Junior, ipo picha aliyopiga mama yake Lulu akiwa na kijana huyo katika pozi la kufanana na mwanaye.
Gazeti hili halikuyaamini maneno ya wadau wala ya mjini, juzi lilimsaka nyota huyo na kumuuliza kuhusu madai hayo ya watu ambapo alikataa katakata kuwa na bwana mpya.
Msikie mwenyewe: “Junior si mpenzi wangu, ni rafiki tu na ana mchumba’ake, sema watu wamekuwa wakinihusisha naye ili niongee wakati mimi sitaki kabisa kuongelea kitu chochote hasa visivyo na maana kama hicho.”
credt: GPL

Recommended

Like Us

Company

Legal Stuff

FAQ's

Blogroll

Subscribe to Newsletter

We'll never share your Email address.
© 2015 Umbeya Specially. Blogger Templates Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.