LAWAMA JUU YA UTEUZI WA KIKOSI CHA TAIF STARS KWA KIM POULSEN - KIBADENI ASEMA WA KULAUMIWA NI MARSH

Unknown     6:33 PM    

Baadhi ya wadau wa soka nchini wamekuwa wakimlalamikia kocha Mkuu wa Taifa Stars Kim Poulsen kwa uteuzi wa timu hiyo, ingawa kocha wa Kagera Sugar, Abdallah Kibadeni 'Mputa' ametamka kuwa wakulaumiwa ni msaidizi wake.

kocha wa Mkuu wa Ruvu Shooting, Boniface Mkwasa hivi karibuni alisema uteuzi wa kocha huyo umeegemea zaidi kwenye klabu za Simba, Yanga, Azam FC na Mtibwa Sugar.
 
Mkwasa alimtaka kocha huyo kujaribu kuwafuatilia wachezaji wa timu nyingine kwani wapo wenye sifa zote za kuichezea timu hiyo na hata kuwazidi baadhi ya waliopo kwa sasa.
 
Kibadeni alisema jijini Dar es Salaam kuwa kocha Kim hapaswi kulaumiwa kwa hilo isipokuwa msaidizi wake ambaye ni Silvester Marsh kushindwa kumshauri.
 
"Kwa upande wangu lawama hizi nafikiri zinapaswa kubebwa na msaidizi wake (Marsh) kwa kushindwa kumshauri mkubwa wake.
"Siamini kama Marsh amewahi kumshauri kitu halafu akakipinga. Kim ni kocha muelewa isipokuwa amekosa mtu sahihi wa kumshauri." alisema Kibadeni.

Katika hatua nyingine nyota wa timu hiyo Themi Felix alisema; "Nafikiri atueleze kuwa kucheza timu ya Taifa Stars ni mpaka uwe Simba, Yanga au Azam FC ndiyo unaweza kuonekana." alisema
Felix ambaye yupo kwenye kiwango kizuri cha soka.

Recommended

Like Us

Company

Legal Stuff

FAQ's

Blogroll

Subscribe to Newsletter

We'll never share your Email address.
© 2015 Umbeya Specially. Blogger Templates Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.