Bayern munich vs Dortmund: wiki kabla ya fainali Dortmund wawakumbusha Bayern machungu ya goli la solskjaer

Unknown     2:21 PM    

Oh no you di'int, Dortmund! (101GG)
Huku zimebakia siku chache kabla ya fainali yao ya Champions League dhidi ya Bayern Munich ndani ya dimba la Wembley, Borussia Dortmund wameanza mind games kwa kuwakumbusha Mabavarian moja ya kumbukumbu zao mbaya kabisa za fainali ya UCL.
BVB wameweka jezi ya Manchester Utd iliyokuwa ikivaliwa na  Ole Gunnar Solskjaer katika jumba lao la makumbusho. Hii itawakumbusha Bayern Munich alichowafanya Mnorway huyo alipofunga goli la ushindi katika dakika ya 93 ya mchezo katika fainali ya mwaka1999 ya Champions League. Tukio hili limekuwa moja ya muhimu katika historia ya michuano hiyo.

Jezi hiyo ni ya Ole Gunnar Solskjaer sio ile aliyoivaa kwenye fainali ya mwaka 99, hii ni ile ambayo alivaa kwenye mchezo wa nusu fainali ya European Cup dhidi ya Dortmund ambapo United walifungwa na Solskjaer - Baby-Faced Assassin alibadilishana na jezi na Knut Reinhard.

Recommended

Like Us

Company

Legal Stuff

FAQ's

Blogroll

Subscribe to Newsletter

We'll never share your Email address.
© 2015 Umbeya Specially. Blogger Templates Designed by Bloggertheme9. Powered by Blogger.